UKWELI KUHUSU MWANAUME ANAVYOCHAGUA MWANAMKE WA KUOA

Unaweza kuwa  ni mzuri kitandani, na ni mrembo sana, na tunaweza kuwa tunalala pamoja kila siku, na tunaweza kuwa tunakukumbuka kila mara .
Hata hivyo, hio sio sababu ya  kutosha ya kumfanya mwanaume akuoe wewe. Ukweli ni kwamba ni kitu kingine kidogo sana , kama hakuna kitu cha kufanya kutokana na hicho.
Sababu kubwa ambayo mwanaume huoa mwanamke hutokea nje ya kitandani , au tuseme nje kama ya chumba cha kulala.  Naona sasa unashangaa jinsi gani sasa naweza kupata mwanaume wa kunioa ?
Rahisi sana, Wanaume wanaoa wanawake ambao wataweza kuwafanya kuwa bora.
Sio bora mwanaume.
Huanzia nje , wanapogundua  bidii yako ya kufanya jambo walipendalo, bila hata ya kuambiwa kufanya, kama vile  usafi. Ina maana ya ndani zaidi ya  neno usafi. Hio huwavuta na kutaka kuchukua jukumu la kutaka kukulinda.
Wanapenda kujua uko wapi,  wanapenda kukujali  wewe na mazingira yako, mfano kujali  usafiri wako, na kama umefika salama, kama una gari.  Na kuna vitu vidogo vidogo ambavyo hata haviwezi kufikirika lakini ni muhimu.
Wanajali jinsi unavyojisikia , sio jinsi unavyoonekana
Kama mwanamke , unaweza kuwa unafikiria,  Ni vitu vizuri na naweza kuvifanya!  Lakini nitavifanyaje vitokee?
Ukweli uko pale , hakuna utakachoweza kukifanya kitokee.Hata kama utaruhusu vitokee.
Ni juhudi, Kwanza na kitu cha muhimu  zaidi, ni kwamba,  mwanaume humpenda  mwanamke ambaye anampenda. Yaani kama ukimpenda, atakupenda. Lakini sio zaidi kama anavyojipenda yeye. Watu wengi huita hilo ni ujasiri.  Lakini ni zaidi ya hilo.
Lakini pia kitu cha kwanza cha kufanya ni  kuruhusu upendo utokee ndani yako; utajisikia vizuri na  utaona kustahili  kwa kujua wewe ni nani.
Kuruhusu upendo maana yake ni  kwamba, wakati  anapokuwa anacheki vitu vyako , kwa mfano gari yako simu yako, notebook yako,  mwachie.  Anapotaka kuondoka na simu yako mwachie,  badala ya kumkatalia kwamba hawezi kushika na wala kuondoka na simu yako.
Kwa mwanaume kuwa mume bora,  huhitaji nafasi na  muda wa kufanya hivyo, kwa  kufupisha.  Mwanaume huoa mwanamke anayemwamini na kwamba atayafanya maisha  yawe mazuri— na zaidi ya uzuri,  Ruhusu hilo litokee kwako.


No comments: