Esma: Diamond, Tanasha ndoa kama kawa!






DADA wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ Esma Khan amefunguka kuwa watu wanao-fikiria ndoa ya kaka yake huyo na mpenzi wake mpya, Tanasha haipo wamechemsha. 

Akizungumza na Showbiz Xtra, Esma alisema kwa sasa kaka yake yuko bize na ziara na ndiyo maana mara nyingi haonekani na mpenzi wake huyo lakini wako vizuri na mpango wa ndoa uko palepale. 

“Sasa yule si ndiyo wifi wa kaka yangu jamani hakuna wa kubadilisha hilo na ndoa ipo kama kawaida tujipange tu kusherehekea na vigoma vya Kigoma,” alisema Esma huku akicheka.





No comments: