Mwanamke Mfanya Usafi Hotelini Aliyeokota Kondomu Yenye Mbegu za Milionea na Kujimiminia Ukeni na Kupata Ujauzito, Ashinda Kesi ya Matunzo ya Mtoto







Mwanamke aliyetambulika kwa jina moja la Jane miaka 40 amevutana Mahakamani na kijana tajiri zaidi jijini Las Vegas baada ya ya mwanamke kutumia mbegu za kiume za milionea huyo alizokuwa amezimwaga kwenye kondomu ndani ya hoteli moja huko. 

Jane alikuwa mfanya usafi ktk hoteli hiyo ndipo alipookota kondomu iliyokuwa imetumika huku ikiwa imejaa mbegu za kiume na akajiiñgizia mbegu hizo kwenye uke wake na bahati nzuri mbegu hizo zikampatia mimba. Wakati huo Jane alikuwa na miaka 36. 

Leo hii analea mtoto mwenye umri wa miaka 4. Katika makabiliano ya kimahakama Jane amekiri kuiba kondomu ya tajiri huyo mdogo mwenye miaka 28 kwani alikuwa akihitaji mtoto. 

Aliiambia mahakama kuwa wakati wa kufanya usafi aliokota Bank statement yenye jina la huyo Tajiri baadae ndipo akaona na kondomu iliyojaa shahawa, aliichukua kondomu hiyo na kujimiminia shahawa ndani ya uke wake. 

Baada ya kufanya hivyo aliacha kazi ya usafi hotelini na alianza kufanya biashara zingine ndogo ndogo huku akilea mimba. 

Vipimo vya DNA vimeonyesha mtoto yule ni wa tajiri huyo na Mahakama imemtaka alipe $2 milioni kwa ajili ya matunzo ya mtoto huyo kwa miaka mitatu iliyopita. 

Mawakili wa tajiri huyo wameapa kukata rufaa dhidi ya mwanamke huyo kwa kile walichodai aliiba majimaji ya mwili wa mteja wao (shahawa) pamoja na kuingilia faragha ya mteja wao. 

Mwanamke huyo alishtaki Mahakamani akidai tajiri huyo hamtunzi mwanaye halali na ameshinda kesi hiyo hivyo kijana huyo tajiri atatakiwa kutoa pesa za matunzo kwa mwanae na zipitie Mahakamani





No comments: