Vitu 7 Viinavyowaboa Wanawake Ukivifanya Mkiwa Kitandani

.



Hakuna mtu anaependezwa na mpenzi anaeboa. Na kwa mioyo yetu ya kiume hakuna sehemu inayotuumiza na kutuacha tumejawa maswali mengi na paniki kede kede kama pale mambo yanapokuwa hayaendi vizuri kitandani.

Kiumeni.com kama jadi yetu ya kukufanya wewe uwe mwanaume bora zaidi, tumekuandalia mambo saba ambayo yanasababisha hali hii itokee na kumfanya mwenza wako aboreke kitandani na kuishia kutoa visingizio vingine visivyokuwa na maana sababu anaona aibu kukwambia. Visome kwa umakini na uvielewe kama unataka wawe wanarudi na kutaka utamu zaidi.

1 – Unaomba ruhusa

Kama ukiwa unauhusiano wa muda mrefu na mwanamke na umeshaelewa lugha yake ya mwili na hisia zake, hakuna kinachomuondoa kwenye hali ya kihisia kama kuombwa ruhusa ya kiofisi kuendelea na jambo hasa juu ya yale mambo yetu mazuri, hauhitaji karatasi ya mahakama ya ruhusa kuendelea kumpa vishawishi na kumtekenya.

2 – Mapenzi ya kukurupuka

Mwanamke wako sio punda wa kupandwa bila matayarisho, hajawa doli la kuchezea. Wanawake wote hupendwa kutayarishwa na kupewa mapenzi ya huba yenye hisia, sio mapenzi ya kikurya “Mama Robhii, raraa ni kurariie!”. Sio kwa staili hii jamaa, jaribu kuwa mvumbuzi wa mambo, ongeza viungo mtoto wa watu alegee na kusisimka kwa huba na mahaba, usiwe na haraka maana tayari yupo kitandani, mmenye kama ndizi kidogo huku unakula taratibu, kidogo tena huku ukiyaachanisha maganda taratibu na kwa staili ndo unakula tena, we ni mpenzi wake na sio mbakajia, mfanye akuone kama malaika ulioshushwa toka mbinguni kwa kazi moja ya kumpenda na kumpa raha duniani.

Usipojiongeza kwenye mambo mazuri ya kitandani, mwingine mjuzi zaidi yako atakupokonya tonge mdomoni.

3 – Haujiongezi inavyopaswa

Japo wanawake wengi huwa ni rahisi kukubaliana na staili ya mapenzi kutokana na wenza wao, ila iwapo kama unatumia staili hio hio kila mkikutana na hamna vionjo vyovyote vinavyobadilika lazima mwenza wako achoke na kuboleka na utendaji wako wa kazi. Kwahio kama ukitaka asikuchoke inabidi ujiungeze na ufanye mabadiliko ya hapa na pale.

Ukifanya kubadilika kila muda utafanya na yeye pia abadilike na kukuonyesha utundu wake wa kike ulipo.

4 – Sehemu moja ya matukio

Kama mwanamke wako unampeleka sehemu moja tu ya tukio, mpaka amekalili jinsi silingi bodi ilipokatikia, upo kwenye matatizo makubwa. Ila mabadiliko ya uwanja yanaweza kutatua hili tatizo hivyo usiwe na wasiwasi. Jaribu kujaribu kufanya matukio hata sehemu ambazo hategemei, mpeleke kwenye sofa, mpeleke bafuni na kama unamaji ya moto patakua patamu huko.

5 – Hautumii maneno au unayatumia kupitiliza

Kutumia sana maneno flani matata kumnongoneza masikioni humfanya mwanamke apandishe mrukhani kwa fujo, ila usitumie maneno yaleyale maana kurudia rudia maneno huyaondolea maana husika na kuyafanya butu. Jaribu kuyatumia katika wakati muafaka na mudi iliyosahihi na fanya uchaguzi mzuri wa maneno matamu yanayoongeza akshi za kimahaba.

6 – Fanya majaribio

Kama upo na mwanamke kwa muda mrefu na unataka mambo chumbani yanoge, unapaswa kubadilisha mikao, jaribu mikao mingine ya kimapenzi, zungumzeni na mwambiane anapendelea nini na angependa kujaribu kipi, mawasiliano ni nguzo kubwa inayoweza kubadilisha mazingira na kufanya staili anayoitamani. Unaweza tumia dawa ya aibu kama Dompo, Sainti Anna au Dodoma Wine.





No comments: