HADITHI: REBEKA ( Zaidi ya Mwanamke) SEHEMU: 01





HADITHI: REBEKA ( Zaidi ya Mwanamke)
SEHEMU: 01

Waumini wa kanisa wote walikuwa kimya wakiendelea kumsikiliza msichana Rebeka aliyekuwa akitoa ushuhuda kwa yale yote aliyoyafanya ambayo yaliyomfanya kila mmoja abakie kinywa wazi wengine bila kutegamea walibubujikwa na machozi.
Baada ya ushuhuda wake wengi waliangua kilio kilichomshtua kila mmoja aliyekuwa mule kanisani wengi wao walikuwa wake za watu walisikika wakisema:
"Oooh! Masikini tumekwisha."
Wengi wao waligaagaa chini kwa kilio cha majuto kwa kweli ulikuwa msiba mkubwa uliokuwa ndani ya kanisa uliompa kazi mchungaji amnyamazishe yupi nani amuache.
Hata waliokuwemo kanisani ilibidi wafanye kazi ya ziada kuwatuliza kina mama waliokuwa wakilia kwa kujitupa chini wengine kufikia hatua ya kujiumiza na kutokwa na damu na wengine kupoteza fahamu.
Ilikuwa ni vigumu kujua nini mahusiano ya ushuhuda wa Rebeka na wale kina mama. Rebeka ambaye alikuwa kama mtu aliyepagawa mikono kichwani machozi yalimwagika kama chemchem ya maji, alijutia kile alichokifanya pale alipojijua..... Ni swali zito kwa msomaji ili kuyajua yote tuungane na mtunzi mahili Ally Mbettu kwenye riwaya hii itakayo kusisimua muda wote na kukupa mafundisho.
*****
Ilikuwa siku ya jumapili Msichana Rebeka alipotumwa na mama yake aende akasanye kuni kwa ajili ya kupikia chakula cha mchana. Hali ya hewa ilitishia kwani kulikuwa na hali ya mawingu iliyoashilia muda wowote mvua itanyesha.
Rebeka alikwenda msituni kuokota kuni huku akimuomba mwenyezi Mungu mvua imuchie kwanza ili aokote kuni kwanza ndio inyeshe. Kutoka kwao hadi msituni ni mwendo wa dakika kumi hadi robo saa.
Akiwa ameshikilia panga mkononi kipande cha kamba na kanga chakavu kwa ajili ya kuwekea ngata ya kubebea kuni. Kila hatua aliyopiga ndivyo wingu lilivyozidi kuwa zito mpaka kuanza kuweka kiza. Lakini hali ile haikumzuia Rebeka kwenda kuokota kuni.
Alifanikiwa kufika msituni bila mvua kudondosha tone la maji na kuanza kuokota kuni ambazo zilikuwa na chache kitu kilichomfanya aingie ndani zaidi ya msitu. Kuni zenyewe zilikuwa moja moja hivyo ilimpa kazi sana kupata mzigo mkubwa.
Akiwa bado anaendelea kutafuta kuni ghafla iliteremka mvua nzito iliyoambatana na upepo mkali. Ukali wa upepo ulimfanya Rebeka ajibanze nyuma ya mti mkubwa ili kusubiri mvua ipungue.
Mvua iliendelea kwa muda wa masaa mawili bila kukatika hata ilipokatika muda ulikuwa umeisha kwenda sana.
Rebeka alikusanya zile kuni zake chache alizookota, lakini zilikuwa zimetota maji ya mvua. Alikuwa hana jinsi alizibeba hivyohivyo na kurudi nazo nyumbani akiwa anatetemeka kwa baridi kali kutokana na nguo zake kulowa na mvua.
Alirudi huku akiwa na hasira za kunyeshewa na mvua na kuni alizozifuata hakuzipata na chache alizopata zilikuwa zimeloweshwa na mvua ambazo zilikuwa hazifai kwa kupikia siku ile. Kibaya zaidi ndani hapakuwa na kuni za ziada za kupikia siku ile.
Alirudi nyumbani akiwa amefura kwa hasira hasa akizingatia asubuhi kifungua kinywa alichokipata kilikuwa cha mkono mmoja alitegemea mchana angalau angedanganya tumbo.
Taratibu aliliacha poli na kuingia sehemu za makazi ya watu huku akiwa amebeba kuni zake chake huku akitetemeka kwa baridi aliona amecheza pata potea kuni hakupata na mvua imemnyeshea.
Akiwa anaelekea maeneo ya nyumbani kwao kabakiza kama nyumba kumi afike kwao alishangaa kusikia jina lake likitajwa tena lile la utani ambalo alikuwa akitaniwa shuleni. Ilimshangaza kwani ilikuwa imeishapita miaka mitatu toka amalize elimu yake ya darasa la saba.
Jina lile lilifia shuleni kibaya zaidi shule aliyokuwa akisoma ni ya kijiji cha sita toka kijijini kwao. Elimu ya msingi aliomea kwa baba yake mkubwa ambaye alimchukua kwa wazazi wake akiwa na miaka sita. Alikuwa na imani pale kijijini hakuna aliyekuwa akilijua jina lake la utani alilokuwa nalo shuleni.
Jina lake la utani aliitwa mama maua kutokana na kupenda kupanda maua kitu kilichopelekea kupewa cheo cha bibi afya. Kabla ya kujibu aligeuka akiwa na kuni zake kichwani kuangalia nani anaye mwita ilikuwa baada ya kumwita midomo minne bila kumjibu mpaka pale alipomtaja jina lake halisi la Rebeka.
Alipogeuka alikutana na mtu ambaye waliachana miaka minne iliyopita ni mmoja wa wanafunzi wenzie lakini alikuwa amemzidi darasa moja. Kabla ya kumaliza yule kijana alikuwa ni kaka mkuu wa shule, alipomfahamu ni nani alitabasamu kwa kumtaja jina lake.
"Aaaah Mabogo!" Rebeka alisema huku akishika mdomo.
"Siamini ni wewe Rebeka mama maua!" Mabogo alisema huku akimchanulia tabasamu pana.
"Ni mimi Mabogo za siku?"
"Nzuri."
"Mmh, na huku unafanya nini?"
"Nikuulize wewe?"
"Mimi huku ndipo kwa wazazi wangu na ndipo nilipozaliwa."
"Hata mimi ni kwetu ila sikukulia huku."
"Umenenepa upo wapi mbona sijakuona hapa kijijini?"
"Nipo mjini tunaganga maisha."
"Hata mimi naona shepu za mjini zinaonekana, shavu dodo!"
"Aaaah kawaida...kwanza pole na mvua ina maana mvua yote imekuishia mwilini?" Mabogo alimuuliza kwa sauti ya huruma.
"Mabogo iishie wapi haya ndio maisha yetu ya kijijini kama mbuzi mbele kamba nyuma kiboko."
"Pole sana."
"Mabogo siwezi kusema asante kwa sababu bado hali hii naendelea nayo wala sina daliliza kujikomboa."
"Samahani Rebeka umeolewa?"
"Niolewe wapi maisha yenyewe kama haya ukimbilie kuolewa si ndio ungekutana na mimi na kunipa shikamoo....Umeisha muona Zawadi?"
"Bado."
"Ukimuona utamsahau mpaka sasa ana watoto wawili na mimba juu ukimuona kama gari zetu za shamba za spilingi kufungia mti wa muhigo najua utajua ni jinsi gani alivyochoka mdomoni kabakia na meno mawili yote yameisha kwa kipigo mumewe mlevi mbwa."
"Una mpango gani na maisha yako?"
"Nikipata nakula nikikosa na lala."
"Sasa Rebeka nisikuweke sana najua kibaridi kinakichonyota nenda nyumbani ila jioni baada ya shughuli zako zote naomba tuonane."
"Nikipata muda, hapa najua siwezi kwenda popote kwa kuwa kuni za kupikia hakuna hivyo lazima nikitoka nitaulizwa ingekuwanimeisha maliza kazi zote na wazazi wangu kwenda kwenye kinywaji hapo huwa na uhuru mkubwa."
"Unataka kuniambia kuni hizi ndizo za kupikia?"
"Nikwambie mara ngapi Mabogo yaani mvua leo imejua kunitenda."
"Basi usihofu nitakusaidia kuni maana jana kama tulijua kulikusanya kuni nyingi kwa ajili ya kuziuza si unajua mdogo wangu ana miradi yake."
"Sasa Mabogo si kuni za biashara?"
"Ndio za biashara lakini nitakulipia mimi."
"Acha tu Mabogo sipendi uhalibu bajeti yako."
"Bajeti nitakuwa nayo mimi na serikali watasemaje...Kwanza Rebeka leo nimefurahi sana kukuona, pokea msaada wangu ili leo mpate kupika chakula cha mchana msaada wangu si kwako tu hata kwa wote walio nyumbani."
"Sawa Mabogo nitashukuru kumbe roho yako ya upendo na huruma ujaiacha."
"Hata wewe msimamo wako haujauacha kweli nimeamini u mwanamke wa shoka imeonyesha jinsi gani pamoja na elimu yako ya msigi lakini amekuwa na upeo wa kuona mbele."
Mabogo aliingia ndani na kutoka na mzigo wa kuni aliomkabidhi, Rebeka alishukuru na kuondoka huku akimuahidi kurudi baadaye.

Inaendelea


  🔞WAKUBWA TU:TAZAMA VIDEO ZA WAKUBWA LIVE UJIONEE STAILI KALI ZA KUMFIKISHA KILELENI MPENZI WAKO




No comments: