Idriss: siwezi kuacha kumpenda Wema



MKALI anayetikisa kunako upande wa Vichekesho Bongo, Idris Sultan amefunguka kuwa hana kinyongo na aliyekuwa mpenzi wake, Wema Sepetu.  Idris ameyasema hayo baada ya kuulizwa kwa nini hajibu komenti zinazo-tolewa na Wema kwenye ukurasa wake wa Instagram kama anavyojibu za wengine kitendo kilichotafsiriwa kwamba anamchukia mrembo huyo.
“Hakuna anaye-weza kuacha kump-enda mtu kabisa, utampata mtu mwingine ambaye utajifunza kumpenda zaidi na yule aliyekuwa wako mwanzoni utajifunza kumheshimu tu. Maisha ni mazuri hasa pale unapokuwa huna kinyongo na mtu hivyo siwezi kuacha kumpenda Wema,” alisema.
STORI: AMMAR MASIMBA




No comments: