Nimeolewa nina watoto wa 2, Mume wangu hunitamkia maneno yanayoumiza sana



Nimeolewa nina watoto 2, mume wangu anapenda kuongea maneno ambayo yananiumiza, kama nimeshakuzalisha sikutaki tena natafuta mpenzi mwingine, najuta kuwa na wewe kuna wanawake warembo zaidi yako. Mume wangu huyu ni mtu mzima 50's na mimi 20's anavyotamka naona anamaanisha nikifikiria mtu mwenye umri wake anajua kitu anachokitaka. Nafikiria kwenda mahakamani kudai talaka. Je, nakosea ?




No comments: