HADITHI: RED BIKINI SEHEMU YA SITA(06).




ILIPOISHIA👉🏽 Mr Kondo akiwa na Farida wakirusha roho mara ghafla mlango ulisukumwa. ENDELEA👇🏽

"Bosi?" Ilisikika sauti ya mlinzi wa geti huku akiwa ameufungua mlango na kuingia ndani. Yule mlinzi aliishia kuita tu kisha akabaki ameduwaa na macho akiyatoa kwa mapozi aliowakuta nayo pale varandani.

"Sa...sa....samahani mkuu." Kisha akarudi nje kwa kasi na mlango akiubamiza.

Huko ndani Mr kondo na Farida walibaki wakivunywa na jasho na kila mmoja  alikuwa akidundwa na moyo wake kuashilia hofu waliyokuwa nayo. Vichwani vyao walijua tayali washafumwa na Happy lakini kwa bahati akaingia mlinzi wa geti.

Baada ya kuganda kwa muda wakiangaliana ndipo kila mmoja akili zikamrudia na kujikuta Mr Kondo akiwa tayali kisha mwaga manii zake kwenye sofa na uume zamani ulikuwa umeshanywea.

"Vipi hawezi kuleta noma?" Mr Kondo alimuuliza Farida huku akisimama na kuanza kukusanya vitu vyake.
"Mmh! Ila hawezi kuleta noma." Farida alijibu.

"Una uhakika?"
"Yeah! Ila we niachie mimi nitajua cha kufanya." Farida aliongea huku akisimama na kuanza kukusanya nguo zake na kuelekea jikoni.

**********
Baada ya siku mbili kijana Edwin alikuwa ameshapata afya na mambo mengine yaliendelea kama kawaida.

"Unajua nini Frola?" Edwin alizungumza.
"I don't know anything." Huku wakiendelea kupiga hatua ndogo ndogo.
"Hivi yule rafiki yako uliyekuwa nae juzi pale cafe anaitwa nani?"
"Mmmh! Edwin!?" Huku akisimama na kumuangalia Edwin kwa mshangao.

"Nini sasa?" Edwin aliuliza.
"Inamaana unamtaka na yule?"
"Sijasema hivyo Mimi."
"Ila?"
"Mbona maswali mengi wakati Mimi nimekuuliza tu ili nimfahamu kama nilivyokufahamu wewe."
"Nani asiyekujua hapa chuoni?"

Edwin alitulia kisha akaanza kutembea taratibu na Frola akimfata kwa pembeni.
"Ukishamfahamu mwishoe?"
"Basi kwani unahisi nini?"
"Mwishoe umrambe nayeye halafu ukae pembeni?" Frola alipozungumza hiyo kauli ghafla simu ya Edwin iliita na mazungumzo yao yalikatishwa kidogo.

"Yes hellow?" Huku akionekana kutega sikio kwa umakini mkubwa.
"Niambie handsome boy?" Ilisikika sauti ya Lecho.

"Am good." Huku akimzuia Frola asiondoke kwa kumshika mkono.
"Vipi sasa? Au umeshasahau?"
"Mmmh! Hapana kwani leo ni lini?" Edwin aliuliza huku akiwa bado kamng'ang'ania mkono Frola.

"Leo bila kukosea ni ijumaa." Lecho alijibu.
"Kwa hiyo unataka kusema weekend inaanzia leo?"
"Exactly!"

Edwin alitulia kidogo kisha akachana kikaratasi kwenye notebook yake na kumkabidhi Frola.
"Niandikie namba yake na jina lake." Aliongea kwa sauti ya chini huku simu yake akiwa ameiweka mbali na mdomo wake. Alipomaliza akairudisha tena sikioni huku akimuangalia Frola.

Frola alionekana kusita kufanya alichoagizwa na Edwin lakini Edwin akampa ishala ya kwamba asijali, ndipo frola akakamata peni na ile karatasi kisha akaanza kuandika namba n jina la Cathe.

Alipomaliza akamkabidhi Edwin ile karatasi kisha akaondoka zake.
"Thank you!" Kwa sauti ya chini ili kusudi Lecho asisikie kwenye simu.

"Mmh kwa hiyo?" Edwin aliuliza.
"Njoo town kwenye lodge moja inaitwa Afrisana lodge nazani utanikuta hapo."
"Afrisana?" Edwin alibaki akijiuliza huku akiwa anawaza kitu.
"Yeah! Vipi kwani?"
"Kwanini tusitafute eneo lingine?" Edwin alijikuta akikumbuka kitu alishawahi kukifanya katika hiyo Lodge. Alishawahi kulala na muhudumua wa hiyo lodge usiku kucha kwa hiyo akienda na Lecho haitaleta picha nzuri.

"Wapi unapopaona panafaa?" Lecho aliuliza.
"Mmmh nazani itapendeza zaidi kama ikiwa One night lodge."
"Ok sio mbaya japo iko nje ya mji."
"Usijali umabli." Edwin alijitutumua huku akionekana kutabasamu kwa kushinda.

"Nipe nusu saa nitakuwa nishafika town na zani tutakutana hapo kuelekea huko"
"Ok! Sawa nakusubilia wewe tu." Lecho baada ya kusema hiyo kauli alikata simu.
"Yes!" Edwin alishangilia huku akiangalia ile karatasi aliyopewa na Frola.

Haraka haraka akaanza kuisevu ile namba kwenye simu yake kisha akaitafuna na ile karatasi.

**********
"Niko njiani nakuja." Alisikika Irene akiongea na mtu kwa simu kisha akakata na kuiweka kwenye mkoba wake.

Baada ya dakika 15 kweli Irene alishuka ndani ya daladala na kuingia ndani ya gari moja ya kifahari na safari ikaanza pale bila kujua ilikuwa ni safari ya kuelekea wapi.

**********
"Kwa hiyo unataka kuniambia ulipanga kweli kutupokonya hiki chumba?" Sudi alimuuliza warden wake ambaye kila siku anamsumbua akihitaji mchezo na yeye.

"Unahisi ningeweza kufanya hivyo?"
"Sijui."
"But..." Akasita kidogo.
"But what?"
"Leo nahitaji twende club nawewe." Huku akilegeza jicho lake.
"Mmmh!" Sudi aliishia kuguna huku akimuangalia Jesca.

"Vipi hujaipenda ofa yangu?"
"Hapana but nahisi niko busy sana."
"Usipange kukataa na usikatae kukubali." Huku alianza kumsogelea aliposimama Sudi.
"Ok! Nimekuelewa, tutaenda."
"Sio tutaenda, sema tunaenda maana muda ndio huu" huku akiangalia saa yake ya mkononi.

Jesca akiwa anazidi kumaogelea Sudi mara kwa fujo mlango ulifunguliwa na Edwin aliongea kama mwendawazimu.

Alipofika ndani kwanza akasita na kushangaa kwa staili alizowakuta wamesimama wale watu kwa maana hata yeye Edwin anajuaga ni jins gani Jesca anamuhusudi sana Sudi.

"Babuuu?" Sudi alimsemesha rafiki yake.
"Vipi babuu?" Huku akiinama chini ya kitanda chake na kuanza kuvuta raba zake za bei ghali kisha akaanza kuvifuta futa na kitambaa chake.

"Babuu unamtoko?" Sudi aliuliza.
"Si unajua mwisho wa wiki huu?"
"Duh! Jamaa hakuna weekend inayokupitaga ndugu yangu."
"Napitwaje kwa mfano?" Edwin aliuliza huku akivua shati yake na kufungua kabati la nguo zake na kutoa fulana moja jeupe na kulitupia kitandani.

Akarudi tena kabatini na kutoa suruali yake aina ya jinzi jeusi na kuitupia kitandani mahali alipotupia fulana yake.

"Jesca? Warden hahahaha maana inabidi tukupe heshima ya cheo chako mama." Edwin alizungumza huku akiwa ananyanyua ndoo ya maji kusudi akaoge bafuni.
"Ndio unaniona?" Jesca aliuliza huku akikaa kwenye kitanda cha Edwin.

Lakini Edwin hakumjibu cha zaidi alitoka na ndoo yake iliyojaa maji na kwenda bafuni huku nyuma akimuacha Sudi akiangaliana na Jesca.
"So! Utabaki peke yako room? Na mwenzako anaenda town?"

"Ok! Nimekuelewa ngoja namimi nijiandae twende wote." Huku akifungua kabati la nguo na kuanza kuchagua viwalo na kuvitupia kitandani kisha akatulia kidogo.

"Vipi?" Jesca aliuliza.
"No!" Huku nayeye akichukua ndoo yake ya kuogea iliyojaa maji na kutaka kutoka, ile anafungua mlango tu na Edwin nayeye akawa anarudi chumbani.

"Mmh! Babuu umeoga au umejimwagia?" Sudi aliuliza huku akimshangaa rafiki yake.
"Babuu kausha basi." Huku akiingia chumbani na kumuacha Sudi akielekea bafuni.

Haraka haraka Edwin alijifuta na kujikausha mwili wake kisha akalitupia taulo lake kitandani pembeni alipokaa Jesca. Akakamata lotion akajipaka mwilini na muda wote huo Jesca alikuwa akimuangalia bila kusema chochote.

Edwin alipomaliza akavuta fualana yake na kuitinga mwilini, kisha akarudi kabatini na kuchukua boxer. Alivua bukta aliyokuwa ameivaa mbele ya Jesca bila kujali chochote baadae akavaa boxer yake na kuchukua jinzi yake kisha akaitinga mwilini.

"Waaaoh! You looking so good." Jesca alishindwa kujizuia ikambidi aseme lake la rohoni.
"Thanks." Edwin alijibu huku akirudisha chupa ya lotion na kutoa saa yake ya mkononi sambba na soksi nyeupe zilizo onekana maridadi sana. Akakaa juu ya meza na miguu akiiweka kwenye kiti na kuanza kuvaa soksi zake huku akionekana mwenye haraka muda wote.

Akavuta raba zake na kuzivaa huku akionekana kujiangalia kila upande juu mpaka chini na alipojiridhisha ndipo akavuta unyunyu wake na kuanza kujipulizia mwilini. Akakusanya kila kitu kilichokuwa chake na kuvifungia kabatini huku akivuta waleti yake iliyojaa noti za elfu kumi kumi na alipozihesabubkwa haraka haraka zilikuwa kama laki mbili hivi.

"Zinatosha sana hizi" alijisemea huku akichukua na ATM kadi yake kwa dharula kama pesa zikimuishia kwa maana mabo ya kula bata huaga hayana adabu.

Alipohakikisha yuko vizuri na hakuna alichosahau ndipo alichukua simu yake na kutuma Ujumbe mfupi kwa Lecho ya kwamba Niko njiani na kuiweka simu yake mfukoni.

Alipotaka kutoka ghafla Sudi nayeye akawa anarejea kutoka maliwatoni na ndoo yake.
"Babuu ndio safari?"
"Mimi ndio nasepa, ila tutajulishana kwa simu kama mambo yako poa."
"Ok poa usiwaze babuu." Huku akienda kuiweka ndoo chini ya uvungu.

**********
Baada ya Masaa mawili kijana Edwin na mwanadada Lecho walikuwa ndani ya lodge ya one night tena wakiwa wamejiachia balaa. Lecho alibaki na kitaiti cha rangi ya pinki huku kifuani akiwa mtupu na kufanya chuchu zake zionekana kwa urahisi na kwa jinsi zilivyokuwa zimesimama basi ilikuwa burudani kwa kijana Edwin kuziangalia kila wakati.

Edwin alibaki na boxer huku kifuani akiwa mtupu na wakiwa wamejilaza kitandani wakiendelea kupata vinywaji vikali vikali na hadithi za hapa na pale huku zikimfanya Lecho awe anacheka muda wote.

"Ngoja kwanza." Edwin alizungumza huku akimpokonya kinywaji Lecho.
"What!?"
"Tukale kwanza then mambo mengine yataendelea." Huku akisimama na kushuka kitandani.

"Ok! Sawa ila nitalipia mimi." Lecho aliongea huku akitoa pesa kwenye mkoba wake na kwakuwa alikuwa anatokea familia ya kitajiri kuhusu pesa kwake hakuna kuwaza waza.

**********
"Kwa hiyo?" Irene alimuuliza mwanababa mmoja aliyekuwa naye mule chumbani na ikionekana ni mpenzi wake wa muda mrefu licha ya kuwa amemzidi umri mbali.

"Si nimekwambia tunaenda kula." Yule mzee alimjibu huku akivaa nguo zake baada ya kukamuana mzunguuko mmoja na mtoto mzuri.

**********
"Unaonaje kabla ya kwenda club twende tukachukue chumba kwanza lodge maana najua tutatoka muda mbaya club na usafiri wa kurudi wewe chuo itakuwa shida sana na Mimi sitoweza kuendesha gari usiku wa manane." Jesca alitoa hoja huku akiwa anapunguza mwendo wa gari yake na kumtazama Sudi usoni.

Walisakanya vyumba pale town lakini hakufanikiwa kupata kwa maana kila lodge unaambiwa vyumba vimejaa, mambo ya weekend hayo watu wanaponda raha kama wako peponi vile.

Gari ilifunga breki mbele ya lodge iliyokuwa nje ya mji iitwayo One night kisha Jesca alishuka huku akifatiwa na Sudi nyuma yake.

Mungu si Athumani wakafanikiwa kupata chumba na wakapelekwa hadi kwenye chumba ña waliporidhishwa nacho wakatulia kwanza chumbani.

"Vipi? Umeridhika nacho?" Sudi alimuuliza Jesca.
"Ndio kiko poa tu." Huku akimkumbatia na kuanza kumnyonya ulimi japo Sudi alionekana kama hafurahishwi na kile kitendo lakini ndio angefanyaje.

Walijikuta wakinohewa na kuamua kukiwasha kwanza kimoja cha kuchangamsha damu hadi suala la kwenda club likafa.

"Njaa inaniuma." Sudi alizungumza huku akiwa amekaa kitandani.
"Ila si kunasehemu ya chakula hapa?"
"Ndio niliiona wakati tunaingia." Sudi alijibu huku akinyanyuka toka kitandani.

Walipovaa nguo zao safari ya kwenda kula ilianza huku Sudi akionekana kana kwamba hafurahii ule uwepo wake pale na sio kwamba Jesca alikuwa ni msichana mbaya? Hapana alikuwa ni msichana mrembo mwenye kila sofa za urembo, basi tu Sudi hakuhitaji kuwa nae.

ITAENDELEA



No comments: